Naibu Waziri wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana
Shonza (mwenye tisheti nyeupe katikati) akiwa katika mazoezi ya jogging na kikundi
cha Kawe Jogging Social Club katika sherehe za miaka mitano ya kikundi hicho
zilizofanyika leo jijini Dar es Salaam (aliyenyoosha kidole kushoto) ni Katibu wa Kawe
Jogging Social Club Bw.Alhaj Seif Muhere.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana
Shonza (mwenye tisheti nyeupe katikati)akifanya mazoezi ya viungo na wanachama
wa vikundi mbalimbali vya jogging mkoani Dar es Salaam katika sherehe za miaka
mitano ya kikundi cha Kawe Jogging Social Club leo,(kushoto) Katibu wa Kawe
Jogging Social Club Bw.Alhaj Seif Muhere na kulia ni Mwanachama wa Jogging Kawe
Social Club Bi Felister Mwijage.
Naibu Waziri wa Wizara ya Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe.Juliana
Shonza akizungumza na wanachama wa vikundi mbalimbali vya jogging Mkoani Dar es
Salaam katika sherehe za maadhimisho ya miaka mitano ya kikundi cha Kawe Jogging
Social Club zilizofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Na Anitha Jonas – WHUSM
Naibu Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza ametoa
wito kwa vijana kujiunga na vikundi vya mazoezi maarufu kama (Jogging Club) kwa
ajili ya kuimarisha afya zao na kujikwamua kiuchumi.
Mheshimiwa Naibu Waziri ametoa wito huo katika sherehe za maadhimisho ya miaka
mitano ya Kawe Jogging Social Club zilizofanyika leo jijini Dar es Salaam ambapo
aliwapongeza wanachama wa Klabu hiyo kwa kuweza kudumu kwa muda wote huo.
“Napenda kuwapongeza kwa juhudi zenu pamoja na ubunifu mliyoutumia katika
kujiongezea kipato kupitia klabu yenu kwa kuanzisha mgahawa ambao unawaongezea
kipato na kukuza uchumi wenu kwa hakika mmekuwa ni mfano wa kuigwa,”Mhe.
Shonza.
Akiendelea kuzungumza katika sherehe hizo Naibu Waziri huyo amewahakikishia
wanaklabu hao ushirikiano pamoja na kushughulikia maombi yao ya kupatiwa mashine
ya maximalipo.
Naye Mwenyekiti wa Kawe Jogging Social Club Bw. Abdul Risasi alimshukuru Naibu
Waziri kwa kujumuika nao katika sherehe hiyo na kutoa ombi la kusaidiwa kupata
mfadhili atakayeweza kuwasaidia kufanikisha ushiriki wao katika mashindano ya
Kilimarathon yanayotarajia kufanyika Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro.
“Tumekuwa tunashiriki katika mashindano ya Kilimanjaro Marathon kwa miaka minne
mpaka sasa na Kawe Jogging Social Club imekuwa ndiyo kikundi pekee nchi nzima
ambacho kimepata nafasi ya kuweza kushiriki mashindano hayo ambapo wanachama
wake hukimbia mpaka kilometa 21,”alisema Bw.Risasi.
Pamoja na hayo Mwenyekiti huyo aliendelea kutoa wito kwa vijana kujiunga katika
vikundi vya jogging kwani kupitia umoja huo wanaweza kujitengeneza fursa za
kiuchumi na kujiongezea kipato badala ya kukaa vijiweni na kulalamikia hali ngumu ya
maisha.
Kwa upande wa mmoja wa wanachama wa Msasani Jogging Club Bi Asha Said alitoa
maoni yake na kusema jogging clubs ni nzuri kwani zinasaidia kupata marafiki pamoja
na kuimarisha afya.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...