Ikiwa Operesheni Lipa Kodi ya Pango la Ardhi inaendelea, ambapo Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi inaendelea kutoa notisi ya siku 14 kwa wadaiwa sugu wa Kodi ya pango la Ardhi huku ikiendelea na kuhabarisha Umma kuhusu umuhimu wa kuzingatia Sheria ya Ardhi Na. 4 ya mwaka 1999, katika vifungu Na. 49 na 51 ambavyo vinadhihirisha ruhusa ya mmiliki kufutiwa umiliki wa ardhi kama mmiliki hatazingatia kulipa Kodi ya Pango la Ardhi.
Kwa upande wake; Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendelea ya Makazi, Dkt Angeline Mabula (Mb), amekuwa akifanya ziara ya kukagua mifumo ya ulipaji kodi ya pango la Ardhi sehemu mbalimbali nchini.

Katika picha ni Naibu Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendelea ya Makazi, Dkt Angeline Mabula (Mb) akikagua mifumo ya ulipaji kodi ya pango la Ardhi sambamba na kuhakiki kumbukumbu za umiliki wa Ardhi Halmashauri ya Wilaya ya Misungwi mkoani Mwanza. Alioambatana nao ni Maafisa Ardhi na Afisa TEHAMA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...