Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi alisema Ujenzi wa Bara bara ya Kinduni, Kichungwani na hatimae kuelekea Kitope unaofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar utasaidia kuharakisha maendeleo ya Wananchi hasa wakulima wa Vijiji hivyo. 

Alisema Ujenzi wa Bara bara hiyo ambao umo ndani ya Ilani ya Uchaguzi ya CCM unatekelezwa kufuatia ahadi iliyotolewa na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mstaafu wa Awamu ya Sita Dr. Amani Karume.

Balozi Seif Ali Iddi alisema hayo wakati akizungumza na baadhi ya Wananchi wa Vijiji vya Kinduni na Kichungwani baada ya kuikagua Bara bara hiyo iliyojengwa na Wahandisi wa Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar katika kiwango cha kifusi kuanzia Kinduni hadi Kichungwani.

Alisema Bara bara hiyo itakapokamilika rasmi itarahisisha mawasiliano ya usafiri kwa Wananchi wa maeneo hayo ambao wengi wao wanajishughulisha na kazi za Kilimo mchanganyiko katika kujipatia riziki zao za kila siku.

Balozi Seif aliwahakikishia Wananchi hao kwamba lengo la Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika hatua ya baadae ya Bara bara hiyo ni kuikamilisha katika kiwango cha lami ili iweze kudumu kwa kipindi kirefu.
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi kati kati akikagua jengo jipya la Skuli ya Msingi ya Kiombamvua lililojengwa na Hoteli ya Kimataifa ya Sea Cliff kutekeleza ahadi za kusaidia huduma na Miradi ya Kijamii.Wa kwanza kulia ni Mshauri muelekezi wa Hoteli hiyo ya Sea Cliff ambae pia ni msimamizi wa Ujenzi wa jengo hilo la Skuli Nd. Yassir De Costa.
Balozi Seif mbae pia ni Mwakilisihi wa Jimbo la Mahonda akikagua Bara bara ya Kinduni iliyopitia Kichungwani na kuelekea Kitope iliyojengwa na Wizara ya Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar katika kiwango cha kifusi.
Balozi Seif akizungumza na baadhi ya Wananchi wa Vijiji vya Kinduni na Kichungwani mara baada ya kuikagua bara bara iliyomo ndani ya Kijiji chao.Kushoto ya Balozi Seif ni Naibu Waziri wa Ujenzi, Mawasiliano na Usafirishaji Zanzibar Mh. Mohamed Ahme Salum na Mbunge wa Viti Maalum Mh.Angelina Adam Malembeka.
Mzee Juma Abdulrahman wa Kijiji cha Kichungwani anayesumbuliwa na maradhi ya macho na Miguu akitoa shukrani kwa niaba ya wanakijiji wenzake mbele ya Balozi Seif kwa hatuanjema iliyochukuliwa na Serikali kuijenga bara bara yao.Picha na – OMPR – ZNZ.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...