Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo akiongoza kikao cha wadau wa kutafuta suluhu ya mgogoro wa matumizi ya ardhi katika Pori Tengefu la Loliondo uliofanyika Kijiji cha Wasso ukiwa ni utekelezaji wa maagizo ya Waziri Mkuu Kassim Majaliwa aliyotoa katika ziara yake hivi karibuni mkoani humo.
Mbunge wa Jimbo la Ngorongoro ambaye ni Naibu Waziri wa Kilimo,Ufugaji na maendeleo ya Uvuvi,William Ole Nasha akizungumza katika mkutano huo ,kushoto ni Mkuu wa mkoa wa Arusha,Mrisho Gambo na Mwenyekiti wa CCM mkoa,Lekule Michael Laizer.
Mkuu wa mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo akipokea nyalaka kutoka kwa Mkazi wa Kijiji cha Wasso, Tina Timan zilizowahi kutumika kutafuta suluhu ya mgogoro huo ambao eneo la Kilometa za mraba 1, 500 lilitengwa kwaajili ya kuruhusu shughuli za uhifadhi ya wanyapori jambo linalopingwa na wenyeji.
Afisa Ardhi wa halmashauri ya wilaya ya Ngorongoro,Kasema Samawa akifafanua namna wilaya hiyo ilivyopanga matumizi bora ya ardhi.
Diwani wa Viti Maalumu katika halmashari ya wilaya ya Ngorongoro,Kijoolu Kakeya akizungumza kwenye kikao kilichowakusanya wadau wote kujadili namna ya kupata suluhu ya mgogoro wa Pori Tengefu la Loliondo mkoa wa Arusha.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...