Na Anthony Ishengoma WAMJW
Msajili wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali NGOs Marcel Katemba amewataka Wasajili Wasaidizi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali nchini kuzisimamia NGOs ili zifanye kazi kwa kuzingatia Sheria na taratibu za nchi.

Ameyasema hayo jijini Dar es Salaam wakati wa kikao kazi cha Wasajili Wasaidizi ili kutoka mafunzo kwa ajili ya kukumbashana majukumu yao Kama wasajili wasaidizi wa Mashirika yasiyo ya Kiserikali.

Amesema kuwa kimsingi Mashirika yasiyo ya Kiserikali bado hayatambui umuhimu wenu hivyo tutawakutanisha na Mashirika haya kwa ajili kufahamiana kiutendaji na kutambuana. 

Aidha Katemba amesema Mashirika yasiyo ya Kiserikali wakati mwingine yanakosa majibu muhimu kutoka kwa Wasajili Wasaidizi  hivyo kusababisha waone kuwa Maafisa Maendeleo ya Jamii sio watu sahihi kusimamia shughuli zao.

"Lengo la Mafunzo haya nikukumbashana mambo muhimu ambayo yatawafanya muweze kutoa majibu stahiki kwa Mashirika haya na kuyasimamia ipasavyo baada ya kujua shughuli wanazozifanya"alisisitiza Bw. Katemba.
 Mkurugenzi wa Idara ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na Msajili wa Mashirika hayo Bw. Marcel Katemba akizungumza na Wasajili Wasaidizi wa Mashirka Yasiyo ya Kiserikali kutoka katika Halmashauri na Wilaya za Mkoa wa Dar es Salaam katika kikao baina yake na Wasajili Wasaidizi hao na wadau wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali kilicholenga kuboresha namna bora ya uendeshaji wa mashirika hayo mkoani humo.
 Baadhi ya Wasajili Wasaidizi wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Mkoani Dar es Salaam wakifuatilia mada na mafunzo mbalimbali yaliyokuwa yakitolea na Msajili wa Mashirika hayo katika kikao kilichowakutanisha kujadili namna bora ya uendeshaji wa mashirika hayo mkoani humo kilichofanyika katika Ukumbi wa Karimjee.
 Mkurugenzi Msaidizi Usajili wa NGOs Bw. Baraka Leonard na Mkurugenzi Msaidizi Ufuatiliaji Bi. Tausi Malima wakijadiliana jambo wakati wa kikao kazi kati ya Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali na Wasajili wasaidizi wa Mashirika hayo mkoani Dar es Salaam kilichofanyika katika Ukumbi wa Karimjee  kilicholenga kuboresha namna bora ya uendeshaji wa mashirika hayo mkoani humo.
 Mkurugenzi wa Msaidizi Idara ya Mashirika Yasiyo ya Kiserikali Bw. Leornald Baraka akiwakumbusha washiriki mambo muhimu yanayohitaji kuzingatiwa kabla na baada ya kusajili Shirika Lisilo la Kiserikali kwa Wasajili wasaidizi wa Mashirika hayo kutoka katika Halmashauri za Mkoa wa Dar es Salaam  katika kikao kilichowakutanisha Msajili wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali, Wasajili Wasaidizi kilichofanyika katika ukumbi wa Karimjee kilicholenga kuboresha namna bora ya uendeshaji wa mashirika hayo mkoani humo.

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...