NA TIGANYA VINCENT, RS-Tabora

MANISPAA ya Tabora kwa kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora imeendesha zoezi la kuwaondoa watu waliovamia eneo la Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Tabora na kufanikiwa kuvunja nyumba zaidi ya 58 za watu waliokuwa wamejenga katika eneo hilo. Hatua hiyo imechukuliwa jana baada ya wahusika kuombwa waondoke kwa hiari kwa kipindi cha zaidi ya mwaka mmoja uliopita lakini walikaidi kutekeleza agizo hilo na kuendelea kuishi katika la Shule hiyo

Akizungumza na waandishi wa habari Mwanasheria kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora Richard Lugomela alisema kuwa wavamilizi hao walipewa taarifa ya kuondoka katika eneo shule muda mrefu ambao unazidi mwaka mmoja lakini wamekuwa wakikaidi kuondoka kwa hiari. Alisema kuwa zoezi hilo ambalo limeanzia katika Shule hiyo lina lengo la kuhakikisha maeneo yote ya Taasisi yalivamiliwa yanarejeshwa na yatumika kwa ajili ya maendeleo yao ili  kutoa huduma bora kwa wananchi.

Lugomela aliongeza kuwa hivi sasa ilikuwa ni vigumu kwa Shule kama Tabora wasichana kuweka miundo mbinu zaidi kwa sababu ya kuwepo kwa wavamizi hao. Alisema kuwa wavamizi hao walipewa taarifa na kuomba wapewe muda wa kujiandaa ili waweze kuondoka lakini badala yake wameendelea kukaa kimya na kupuuzia agzio la kuwataka kuondoka katika eneo walilolivamia.

Alitoa wito kwa watu wengine wanaojijua kuwa wamevamia maeneo ya Taasisi nyingine za elimu kama vile Shule ya Sekondari Milambo, Tabora wavulana na hata yasiyokuwa yao kuanza kuondoka wao kwa hiari yao la sivyo watalazimika kulipia gharama za uvunjaji wa nyumba zao endapo Serikali itatekeleza zoezi la kuwaondoa. Lugomela alisema kuwa eneo hilo lilitengwa na Serikali kwa ajili ya matumizi ya Shule ya Wasichana toka mwaka 1958 na pia katika sehemu hiyo lipo eneo ambalo ni chanzo cha maji.

Kwa upande wa Mhandisi wa Maji wa Manispaa ya Tabora Mohamed Almasi alisema kuwa watu waliojenga katika eneo hilo hawana vibali vya ujenzi na hivyo ni wavamili ambao walipaswa kuwa wameshaondoka siku nyingi. Alisema kuwa baada ya kumalizika kwa zoezi la kuwaondoa wavamizi hao katika shule hiyo ya wasichana ya Tabora watahamia katika maeneo mengine ya Taasisi na kwa watu binafsi ambao maeneo yao yamekaliwa na watu wengine kinyume cha sheria.

Almasi alitoa wito kwa wakazi wa Manispaa ya Tabora wanaotaka kujenga wapelekea ramani zao katika Manispaa ya Tabora ili waweze kupatiwa kibali cha ujenzi kabla ya kuendeleza maeneo yao. Mmoja wa waathirika wa bomoa bomoa Hawa Katabi alisema kuwa hakupata taarifa ya zoezi hilo jambo liliwafanya washindwe hata kuondoa mabati na matofauli.

Alisema ni vema zoezi hilo linapotaka kufanyika wakapewa muda wa kutosha ili waweze kuokoa mali zao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...