Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla amefuta vibali vyote vilivyotolewa na Wizara yake vya Uwindaji wa makampuni ili kuwa na utaratibu mpya wa uombaji kwa njia ya mnada.

Waziri Dk.Kigwangalla ametoa agizo hilo jana jioni wakati wa kuhitimisha mazungumzo yake na wadau mbalimbali wa sekta ya Utalii na Maliasili aliokutana nao mjini hapa Dododma.

“Kwa mamlaka niliyonayo. Natamka kwamba, nafuta rasmi vibali vyote vya Uwindaji kwa makampuni vilivyotolewa na wizara yangu kwa mwaka huu. Pia naagiza Watendaji wote wanaosimamia ili, wahakikishe wanaandaa mchakato ndani ya siku 60 ili mchakato huo wa mnada ufanyike na uwe wa uwazi” alieleza Dkt. Kigwangalla.

Pia ametoa onyo na maagizo mazito kuhakikisha kuwa vitalu vyote vyenye migogoro ikiwemo vile vya Loliondo, Natroni na maeneo mengine kutotolewa kwa vibali vya uwindaji mpaka hapo watakapokamilisha tatizo la migogoro hiyo.
Aidha, ametoa agizo kwa hoteli 10 zilizobinafsishwa kutoka Serikalini zirejeshwe ndani ya siku 60 kuanzia sasa huku akiagiza watendaji waandike barua kwa msimamizi wa hazina.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...