Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Prof. Frolens Dominic Andrew Makinyika Luoga kuwa Gavana wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT).
Prof. Luoga anachukua nafasi ya Prof. Benno Ndulu ambaye anamaliza muda wake.
Prof. Luoga ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Taaluma).
Mhe. Rais Magufuli ametangaza uteuzi huu leo tarehe 23 Oktoba, 2017 katika hafla ya kuwatunuku vyeti vya shukurani na pongezi wajumbe wa kamati zilizofanya uchunguzi wa aina, kiwango na thamani ya madini yaliyokuwemo katika makinikia, iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Katika hafla hiyo Mhe. Rais Magufuli amewatunuku vyeti wajumbe wote 28 wa kamati hizo kwa kutambua mchango mkubwa wa kila mmoja wao katika uchunguzi na majadiliano kuhusu rasilimali za madini na matokeo ya kazi yao ambayo yameiletea nchi na Serikali faida na heshima kubwa.
Prof. Luoga anachukua nafasi ya Prof. Benno Ndulu ambaye anamaliza muda wake.
Prof. Luoga ni Naibu Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (Taaluma).
Mhe. Rais Magufuli ametangaza uteuzi huu leo tarehe 23 Oktoba, 2017 katika hafla ya kuwatunuku vyeti vya shukurani na pongezi wajumbe wa kamati zilizofanya uchunguzi wa aina, kiwango na thamani ya madini yaliyokuwemo katika makinikia, iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam.
Katika hafla hiyo Mhe. Rais Magufuli amewatunuku vyeti wajumbe wote 28 wa kamati hizo kwa kutambua mchango mkubwa wa kila mmoja wao katika uchunguzi na majadiliano kuhusu rasilimali za madini na matokeo ya kazi yao ambayo yameiletea nchi na Serikali faida na heshima kubwa.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...