Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania amewataka wataalamu wa masuala ya lishe na urutubishaji chakula kuwa mstari wa mbele katika kutoa elimu ya virutubisho kwa wananchi.

Makamu wa Rais ameyasema hayo leo wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa siku mbili wa Kitaifa kuhusu Urutubishaji Chakula uliofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere, Jijini Dar es Salaam.

Mhe. Samia Suluhu alisema ukosefu wa upatikanaji wa vyakula vyenye virutubisho   unaweza kuathiri Taifa hasa wakati huu nchi inapolekea kuwa Tanzania ya viwanda, Alielekeza ushirikishwaji na wadau malimbali katika kukabiliana na changamoto utasaidia kupunguza tatizo hili , takwimu zinaonyesha hali yetu ya lishe bado hairidhishi ila ni vyema kuweka nguvu pamoja ili watoto wetu ambao ni Taifa la Kesho waweze kujenga Taifa imara.

Makamu wa Rais alisema Tanzania ina asilimia 34 ya watoto wenye udumumavu pamoja na magonjwa mengine kama mgongo wazi na vichwa vikubwa kutokana na lishe duni.Makamu wa Rais alisema atakuwa na mkataba na Wakuu wote wa mkoa kuhakikisha kila mkoa unaweka takwimu zake vizuri na jitihada wanazofanya kuelimisha wananchi wao umuhimu wa lishe bora na virutubishi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akihutubia wakati wa ufunguzi wa Mkutano wa Taifa wa Urutubishaji wa Chakula uliofanyika kwenye kituo cha Mikutano Cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
 Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akikata keki iliyopikwa kwa unga wa mahindi wenye vitamini A na ngano mara baada ya ufunguzi wa Mkutano wa Taifa wa Urutubishaji wa Chakula uliofanyika kwenye kituo cha Mikutano Cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na watoto waliozaliwa na tatizo la vichwa vikubwa na mgongo wazi (Hydrocephalus and Spina Bifida) na wazazi wao wakati ufunguzi wa Mkutano wa Taifa wa Urutubishaji wa Chakula uliofanyika kwenye kituo cha Mikutano Cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar Es Salaam. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais).

KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...