TSN Group Tanzania, katika kuhakikisha inatoa huduma bora kwa wateja wake hapa nchini, imeingia mkataba na MIMOSA CONCIERGE inayotoa MIMOSA Black Card ambayo ni kadi maalum kwa wateja wanaofika kupatiwa huduma kupitia kadi hizo. 

Akizungumza na waandishi wa habari wakati wa kusaini mkataba huo na kampuni hiyo jijini Dar es Salaam, leo Meneja Masoko wa TSN alisema, Jahu M. Kessy amesema TSN imelenga kuongeza tija katika kutoa huduma zake.
 “Tunarahisisha na kuboresha huduma zetu kuwa bora na za kisasa. Pengine huduma hii itapanua wigo wa wateja wetu watumiao Black Cards kwa Dar es salaam lakini kwa Mwanza TSN Hypermarket inakuwa kampuni ya kwanza kupokea na kukubali malipo kupitia Black card ya Mimosa. Hatua ambayo ni kubwa kuchukuliwa na TSN katika kuwajali wateja wake.”
 “Sasa ukifanya malipo kupitia kadi ya Mimosa kwenye supermarket zetu na Petrol station unajiweka katika nafasi ya kushinda punguzo la zaidi ya asilimia 5 pamoja na kuponi ya zawadi wa kwateja watakao tumia kiasi cha shillingi laki moja kwa manunuzi ya mara moja,” alisema Jahu. 

Akieleza zaidi juu ya huduma na faida wazipatazo wateja watumiayo kadi hizo, Mkurugenzi Msiaidizi wa MIMOSA, Leonce Mongi alisema kupitia kadi hii Mteja wa TSN hatapata tu punguzo la bei kutoka TSN pekee lakini pia atapata offer mbalimbali zitokanazo na kadi hiyo kupitia discount partners wengine ambao ni zaidi ya watoa huduma 71 Nchi Nzima.  
 Jahu alisema TSN inajiimarisha katika kutoa huduma zake kwa wateja, kuwasikiliza na kuwasaidia, hivyo basi kuona umuhimu wa kuwapatia wateja wake wenye MIMISA black card nafasi ya kufanya malipo yao kwa uhuru na furaha. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...