NA VICTOR MASANGU,
KIBITI
UONGOZI wa halmashauri mpya ya Wilaya ya Kibiti Mkoani Pwani
imeanza kutekeleza maagizo yaliyotolewa Naibu waziri ofisi ya Rais Tawala za
mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo ya kuhakikisha wanaboresha
sekta ya afya hususan katika maeneo ya Delta kwa kununua vifaa tiba, madawa,
pamoja na vitanda maalumu kwa ajili ya kujifungulia wakinamama wajawazito.
Akizungumza na waandishi wa habari katika mahojiano maalumu kuhusina na
utekelezaji wa maagizo hayo ya naibu Waziri Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Alvera
Ndabagoyo alisema kuwa kwa sasa tayari wameshaanza kununua vifaa mbali mbali
katika zahanati ili kuweza kuboresha
huduma kwa wagonjwa wanaokwenda kupatiwa matibabu.
Alvera alisema kwamba hapo awali katika sekta ya afya hasa
kwa upande wa wananchi waliokuwa wanaishi
maeneo ya visiwani (Delta) walikuwa wanakabiliwa na changamoto ya upatikanaji wa huduma ya afya kwa kipindi
kirefu kutoka na sehemu zenyewe ufikaji wake kuwa ni mgumu kutokana na kutumia usafiri wa majini.
“ Ni kweli hivi karibuni Naibu Waziri ofisi ya Rais Seleman
Jafo alifanya katika Wilaya yetu mpya ya Kibiti, na kuweza kukagua miradi mbali
mbali ya maendeleo na kujionea changamoto zinazowakabii wananchi,hivyo
alituagiza sisi kama watendaji tujipange na kuweza kuzitafutia ufumbuzi wa
kudumu changamoto hizo,hasa katika sekta ya afya na kimsingi tumefanikiwa kwa
kiasi kikubwa kununua mambo muhimu ambayo yanahitajika kwa wananchi
wetu,”alisema Mkurugenzi huyo.
Alibainisha kuwa licha ya Wilaya hiyo ya Kibiti kuwa ni mpya
lakini uongozi wa halmashauri hiyo wameshaanza kuweka mikakati kabambe kwa
ajili ya kuweza kuleta mabadiliko chanya ya kimaendeleo kwa wananchi wao katika
maeneo mbali mbai ikiwemo sekta ya afya,
elimu, miundombinu pamoja na maji ili
kuweza kuwasogezea huduma kwa ukaribu.
Pia Mkurugenzi huyo alisema moja ya jitihada ambazo
wamekwisha zifanya ni pamoja na kupeleka nishati ya umeme wa Solar power katika
zahanati ya Salale,kupeleka kitanda maalumu kwa ajii ya kujifungulia kinamama
wajawazito katika zahanati ya Mchinga ikiwa sambamba na kupeleka Solar Power
nyingine katika zahanati ya Mfisini.
Kadhalika alisema nia na madhumuni yao makubwa ni
kuhakikisha wanatekeleza maagizo yote yaliyotolewa na Naibu waziri hasa kwa kuwaangalia
zaidi wananchi wa maeneo ya vijijini na wale wanaoshi sehemu za Delta katika
kuwafikishia huduma mabli mbali wanazostahili.
HIVI karibuni Naibu Waziri ofisi ya Rais Seleman Jafo
alifanya ziara yake ya kikazi katika Wilaya mpya ya Kibiti na ambapo aliweza
kubaini kuwepo kwa changamoto mbali mbali katika sekta ya afya, elimu, maji,
miundombinu, usafiri, hivyo aliagiza uongozi wa halmashauri hiyo kuweza
kuzitatua haraka iwezekanavyo ili kuweza
kuwapa fursa wananchi waweze kufanya shughuli za maendeleo bila ya kuwa na
vikwazo.
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo kushoto akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Kibiti Ally Ungando wakati alipofanya ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwa sambamba na kubaini changamoto mbali mbali zinazowakabili.
Naibu Waziri ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo kulia akizungumza na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Alvera Ndabagoyo wakati alipofanya ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua shughuli za kimaendeleo pamoja na kubaini changamoto zinazowakabili wananchi(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Naibu Waziri Ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo kushoto akiteta jambo na Mbunge wa Jimbo la Kibiti Ally Ungando wakati alipofanya ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua miradi mbali mbali ya maendeleo ikiwa sambamba na kubaini changamoto mbali mbali zinazowakabili.
Naibu Waziri ofisi ya Rais Tawala za mikoa na serikali za mitaa (TAMISEMI) Seleman Jafo kulia akizungumza na Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya Wilaya ya Kibiti Alvera Ndabagoyo wakati alipofanya ziara yake ya kikazi kwa ajili ya kukagua shughuli za kimaendeleo pamoja na kubaini changamoto zinazowakabili wananchi(PICHA NA VICTOR MASANGU)
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...