Wanawake wanaoshiriki katika mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) unaoendeshwa na Kampuni ya AFREXA International Ltd, wametakiwa kufahamu haki mbalimbali za binadamu zinamwongoza mwanadamu kushiriki vyema katika shughuli za kimaendeleo.

Akizungumza Jijini DSM, wakati wa semina ya siku moja ya wanawake kuelekea katika mafunzo ya kuendesha vyombo vya moto vya biashara, mwanasheria kutoka Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) WIGAYI KISSANDU amesema ni muhimu kwa wanawake kufahamu haki hizo kwa kuwa zinatoa mwongozo kufikia malengo.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mkuu Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) MARTIN GABONE amesema semina hiyo ni moja ya hatua za mwanzo za mafunzo ya udereva kwa wanawake kwa ajili ya kuendesha vyombo vya moto vya biashara na kusisitiza wanawa wajibu wa kuhakikisha wanawake hao wanaingia rasmi katika sekta ya usafirishaji kwa kuajiriwa au kujiajiri.

Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) hadi sasa umesajili zaidi ya wanawake 200 kutoka maeneo mbalimbali nchini, ili waweze kuwapatia bure mafunzo ya udereva wa vyombo vya moto vya biashara ambapo baada ya mafunzo hayo watatafutiwa ajira na wengine watawezeshwa ili waweze kujiajiri.

Martin Gabone-Mkurugenzi Mkuu Mradi wa Wanawake Kwenye Usukani (WOW) akifungua semina ya mafunzo ya haki za wanawake wanaoshiriki katika mradi huo iliyofanyika mwishoni mkwa wiki Kinondoni jijini Dar es salaam.
WIGAYI KISSANDU-Mwanasheria Kituo cha Msaada wa Sheria kwa Wanawake (WLAC) akitoa mafunzo katika semina hiyo.
Baadhi ya washiriki wakiwa katika semina hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...