Jeshi la Polisi Mkoani Geita limekanusha taarifa ya kukamatwa kwa Waziri mkuu mstaafu ambaye pia ni mjumbe wa kamati kuu Taifa ya chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema Mhe. Edward Lowassa.
Kufutia taarifa ya kukamatwa kwa Mhe. Lowassa zilizosambaa mitandaoni, Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoani Geita Mponjoli Mwabulambo (pichani) alisema kwamba walimzuia kwa sababu za kiusalama na kwamba walilenga katika suala la ulinzi wa jamii na usalama wa wao wenyewe na si vinginevyo.
“Kwa Kiswahili kizuri ni kwamba tulikuwa tumemzuia...Hatukuwa tumemkata. Tulikuwa tumezuia ule msafara wake kwa ujumla. Nyuma ya kumzuia kwake lilikuwa ni suala la usalama na ulinzi kwa ujumla na si vinginevyo”, alisema Mwabulambo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...