Mkutano Mkuu wa Chama cha Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania (TAFCA) Mkoa wa kisoka wa Kinondoni utafanyika Februari 18 mwaka huu jijini Dar es Salaam katika ukumbi utakaotangazwa baadaye.

Mbali ya ajenda za Kawaida za kikatiba, Mkutano huo utaoongozwa na Mwenyekiti wake Eliutery Mholery utapanga tarehe ya uchaguzi ya Kamati mpya ya Utendaji baada ya iliyopo kumaliza muda wake.
Pia Mkutano huo utazungumzia uanzishaji wa Chama cha Makocha cha Wilaya mpya ya Ubungo ambayo imemegwa kutoka Wilaya ya Kinondoni.

Tayari Wilaya ya Ubungo imeshasajili na kufanya uchaguzi wa viongozi wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Ubungo (UFA).
Tunatoa mwito kwa makocha wote wa TAFCA Kinondoni kuhudhuria Mkutano huo muhimu kwa ustawi wao pamoja na mpira wa miguu kwa wilaya za Kinondoni na Ubungo.

Boniface Wambura MGOYO
Mjumbe Kamati ya Utendaji TAFCA Kinondoni

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...