Na Dotto Mwaibale.

WAHARIRI wa vyombo vya habari wamekutana katika mkutano maalumu wa siku mbili kwa ajili ya kujadili mambo kadhaa yanayohusu tasnia hiyo nchini.

Akizungumza wakati akifungua mkutano huo Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Theophil Makunga alisema mkutano huo utawajumuisha wadau wa sekta ya habari kutoka ndani na nje ya nchi.

"Tumewaalika wenzetu wa nje ili watupe uzoefu wa jinsi wanavyofanya katika tasnia ya habari katika nchi zao" alisema Makunga.

Alisema katika mkutano huo ambao unafanyika Hoteli ya Protea Court Yard mambo yatakayo zungumziwa ni kupitia sheria ya huduma ya vyombo vya habari iliyopitishwa na Bunge na kusainiwa na Rais Dk. John Magufuli pamoja na kujadili mpango mkakati wa Jukwa la Wahariri wa kuendeleza tasnia ya habari nchini.

Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura alisema ni muhimu kwa wanahabari kuwa na mpango mkakati wa miaka 10 ili kupata majibu sahihi ya tasnia hiyo.
 Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF) Theophil Makunga (kulia), akizungumza Dar es Salaam leo wakati akifungua mkutano wa siku mbili wa wahariri  kupitia sheria ya huduma ya vyombo vya habari uliyopitishwa na Bunge pamoja na kujadili mpango mkakati wa TEF wa kuendeleza tasnia ya habari nchini. Kushoto ni Makamu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile na Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura.
 Mkurugenzi Mtendaji wa Mfuko wa Habari Tanzania (TMF), Ernest Sungura.
 Makamu Mwenyekiti wa TEF, Deodatus Balile akizungumza kwenye mkutano huo.
 Taswira ndani ya ukumbi wa mkutano huo
Wahariri ndani ya chumba cha mkutano.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...