Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii

Jumla ya Vikundi 16 kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini vinavyojihusisha na masuala ya kilimo vimekutanishwa na Tasisi za kifedha na mabenki ili kuwezeshwa kama mpango wa taasisi ya Land O Lakes.

Akizungumza na Globu ja Jamii,Mshauri wa biashara bunifu kutoka tasisi hiyo ,Renalda Lema amesema kuwa katika vikundi hivyo 16 wamewakilishwa na watu wawili wawili,ili kuwasilisha ubunifu wao kwa taasisi hizo na kupata fursa ya kupanua biashara yao.

“Kama ambavyo unaweza kuona wabunifu walivyotengeza mashine mbalimbali, ambazo zitaweza kumuondoa mkulima kutoka sehemu moja hadi nyingine, hasa katika serikali hii ambayo inahamasisha uchumi wa viwanda, hivyo sisi tumeona uchumi wa viwanda hauwezi kufanikiwa bila ya kuanza kuwawezesha wakulima katika hatua ya awali kabisa” amesema Renalda.

Ametoa wito kwa wadau na taasisi mbalimbali ambazo zinahitaji kuwawezesha wakulima hao kwa namna moja ama nyingine,kuwasiliana na taasisi ya Land O’ Lakes kuwakutanisha na wakulima hao.
Mkurugenzi wa tasisi ya fedha ya Brac, Mahufuzii Ashrafu , akizungumza na baadhi ya wabunifu waliokutanishwa na kampuni hiyo ili waweze kuwezeshwa kama mpango wa tasisi ya Land O Lakes ili waweze kufikia malengo waliyojiwekea.
Mbunifu wa mashine ya kukamua matunda kutoka mkoa wa Songwe, Yohana Mwanzyunga(wa kwanza kulia) akiwaonyesha washiriki wengine mtambo wa kukamua matunda.
Baadhi ya washiriki wakiangalia mashine ya kupukucha halizeti

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...